Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi, akizungumza wakati akifungua Maadhimisho ya Siku ya Vinasaba Tanzania 2026 yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete, Dodoma Aprili 23, 2026.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Christopher Kadio, akizungumza kwenye ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku ya Vinasaba Tanzania kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kufungua maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete, Dodoma Aprili 23, 2026.
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko akitoa utambulisho wa viongozi na wadau mbalimbali wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku ya Vinasaba Tanzania 2026 yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete, Dodoma Aprili 23 - 24, 2026.
Profesa Edda Vuhahula, kutoka Chuo Kikuu cha Kairuki, akiwasilisha mada kuhusu masuala ya Vinasaba kwenye Maadhimisho ya Siku ya Vinasaba Tanzania 2026 yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete, Dodoma Aprili 23 - 24, 2026.
Meneja wa Maabara ya Sayansi jinai Baiolojia na vinasaba, Dkt. Fidelis Bugoye kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali akiwasilisha mada kuhusu masuala ya Vinasaba kwenye Maadhimisho ya Siku ya Vinasaba Tanzania 2026 yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete, Dodoma Aprili 23 - 24, 2026.
Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi (aliyekaa katikati), akiwa pamoja na Viongozi wa Wizara ya Afya, Mamlaka na Mkemia Mkuu wa Serikali wa Zanzibar na baadhi ya washiriki na Wadhamini wa Maadhimisho ya Siku ya Vinasaba Tanzania 2026 baada ya ufunguzi wa maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete, Dodoma Aprili 23, 2026.
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko, akizungumza wakati akifungua mafunzo ya Kanzidata ya Maktaba kwa watumishi wa Makao Makuu na Ofisi ya Kanda ya Kati (hawapo pichani), yaliyofanyika katika ukumbi wa Dkt. Mafumiko Dodoma, Aprili 2, 2026.
Mkuu wa Kitengo cha Udhibiti Ubora na Usimamizi wa Vihatarishi, Benny Mallya, akiongea kabla ya kumkaribisha Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko, (hayupo pichani) kufungua mafunzo ya Kanzidata ya Maktaba kwa watumishi wa Makao Makuu na Ofisi ya Kanda ya Kati yaliyofanyika katika ukumbi wa Dkt. Mafumiko Dodoma, Aprili 2, 2026.
Baaadhi ya watumishi wa Mamlaka, Makao Makuu na Ofisi ya Kanda ya Kati, wakifuatilia wasilisho katika mafunzo ya Kanzidata ya Maktaba yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Dkt. Mafumiko Dodoma, Aprili 2, 2026.
Msimamizi wa Maktaba, Nuriati Hamisi akiwasilisha mada juu ya jinsi ya kutumia Kanzidata mbalimbali za maktaba kwa Watumishi wa Mamlaka Makao Makuu na Ofisi ya Kanda ya Kati (hawapo pichani) kwenye mafunzo ya Kanzidata ya Maktaba yaliyofanyika katika ukumbi wa Dkt. Mafumiko Dodoma, Aprili 2, 2026.