Mkemia Mkuu wa Serikali Dkt. Fidelice Mafumiko, akizungumza wakati akifunga mkutano Mkuu wa mwaka wa Wakaguzi wa Kemikali na Maabara za Kemia (hawapo pichani), mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Arusha Corridor Spring Juni 5-6, 2026.
Mkurugenzi wa Huduma za Udhibiti, Daniel Ndiyo akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkemia Mkuu wa Serikali Dkt. Fidelice Mafumiko (hayupo pichani), kufunga mkutano Mkuu wa Mwaka wa Wakaguzi wa Kemikali na Maabara za Kemia mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Arusha Corridor Spring Juni 5-6, 2026.
Baaadhi ya Wakaguzi wa Kemikali na Maabara za Kemia, wakifuatilia ajenda mbalimbali zilizowasilishwa katika mkutano Mkuu wa mwaka wa Wakaguzi wa Kemikali na Maabara za Kemia uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Arusha Corridor Spring Juni 5-6, 2026.
Meneja wa Mamlaka, Ofisi ya Kanda ya Kaskazini, Eliamini Mkenga, akizungumza wakati akitoa neno la kuwaaga Watumishi wa Mamlaka katika mkutano Mkuu wa Mwaka wa Wakaguzi wa Kemikali na Maabara za Kemia uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Arusha Corridor Spring Juni 5-6, 2026.
Meneja wa Mamlaka, Ofisi ya Kanda ya Ziwa, John Wanjala akizungumza na wasimamizi wa kemikali kutoka Kanda ya Ziwa (hawapo pichani), wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa wasimamizi hao yaliyofanyika kuanzia Mei 19 hadi 20, 2026, mkoani Mwanza.
Mshiriki wa mafunzo ya usimamizi salama wa kemikali akiuliza maswali wakati wa uwasilishaji wa mada mbalimbali.
Wasimamizi wa Kemikali kutoka mkoani Mwanza, wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wataalam kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Kanda ya Ziwa (hawapo pichani), katika siku ya kwanza ya mafunzo.
Meneja wa Mamlaka Ofisi ya Kanda ya Ziwa, John Wanjala (aliyesimama), akielezea majukumu mbalimbali ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali pamoja na kuelezea Sheria na Kanuni za Udhibiti na Usimamizi wa Kemikali za Viwandani na Majumbani kwa wasimamizi wa kemikali walioshiriki mafunzo ya usimamizi salama wa kemikali yaliyofanyika jijini Mwanza, Mei 19, 2026.
Mtumishi wa Mamlaka, Boaz Mizar akitoa elimu kuhusu utambuzi na mawasiliano ya kemikali hatarishi na kadi ya usalama wa kemikali kwenye mafunzo kwa wasimamizi wa kemikali, Mei 19, 2026, mkoani Mwanza.
Mtumishi wa Ofisi ya Kanda ya Ziwa, Mathias Shamba kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali akiwasilisha mada kuhusu Taratibu za Usajili wa Makampuni yanayojishughulisha na kemikali.