Meneja wa Mamlaka, Ofisi ya Kanda ya Ziwa, John Wanjala akizungumza na wasimamizi wa kemikali kutoka Kanda ya Ziwa (hawapo pichani), wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa wasimamizi hao yaliyofanyika kuanzia Mei 19 hadi 20, 2026, mkoani Mwanza.
Mshiriki wa mafunzo ya usimamizi salama wa kemikali akiuliza maswali wakati wa uwasilishaji wa mada mbalimbali.
Wasimamizi wa Kemikali kutoka mkoani Mwanza, wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na wataalam kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Kanda ya Ziwa (hawapo pichani), katika siku ya kwanza ya mafunzo.
Meneja wa Mamlaka Ofisi ya Kanda ya Ziwa, John Wanjala (aliyesimama), akielezea majukumu mbalimbali ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali pamoja na kuelezea Sheria na Kanuni za Udhibiti na Usimamizi wa Kemikali za Viwandani na Majumbani kwa wasimamizi wa kemikali walioshiriki mafunzo ya usimamizi salama wa kemikali yaliyofanyika jijini Mwanza, Mei 19, 2026.
Mtumishi wa Mamlaka, Boaz Mizar akitoa elimu kuhusu utambuzi na mawasiliano ya kemikali hatarishi na kadi ya usalama wa kemikali kwenye mafunzo kwa wasimamizi wa kemikali, Mei 19, 2026, mkoani Mwanza.
Mtumishi wa Ofisi ya Kanda ya Ziwa, Mathias Shamba kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali akiwasilisha mada kuhusu Taratibu za Usajili wa Makampuni yanayojishughulisha na kemikali.
Meneja wa Mamlaka, Ofisi ya Kanda ya Ziwa, John Wanjala (katikati), akiwa pamoja na washiriki wa mafunzo ya usimamizi salama wa kemikali baada ya kufungua mafunzo ya siku mbili kwa wasimamizi wa kemikali yaliyofanyika kuanzia Mei 19 hadi 20, 2026, jijini Mwanza.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akitoa hotuba mbele ya Wafanyakazi (hawapo pichani) katika maadhimisho ya siku ya Wafanyakazi duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Njombe Mei 1, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasalimia Wafanyakazi (hawapo pichani) baada ya kuwasili mkoani Njombe katika maadhimisho ya siku ya Wafanyakazi duniani ambayo kitaifa yalifanyika mkoani Njombe Mei 1, 2026.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, akizungumza mbele ya Wafanyakazi (hawapo pichani) katika maadhimisho ya siku ya Wafanyakazi duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Njombe Mei 1, 2026.