Kamishna Msaidizi wa Polisi, G.J Kessy, kutoka Chuo cha Polisi – Kidatu, akizungumza wakati akifungua mafunzo ya usimamizi wa sampuli za jinai kwa wanafunzi wa Shahada na Stashahada ya Polisi (hawapo pichani), katika mafunzo yaliyofanyika katika Chuo cha Maafisa Polisi Kidatu- mkoani Morogoro, Februari 6, 2026.
Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Mohamed Mdemu, kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, akizungumza na wanafunzi wa Shahada na Stashahada ya Polisi (hawapo pichani) wakati wa kuwakaribisha kwenye mafunzo ya usimamizi wa sampuli za jinai yaliyofanyika katika Chuo cha Maafisa wa Polisi Kidatu- mkoani Morogoro, Februari 6, 2026.
Meneja wa Maabara ya Sayansi Jinai Baiolojia na Vinasaba, Dkt. Fidelis Bugoye, akiwasilisha mada kuhusu namna ukusanyaji, uhifadhi, usafirishaji na utunzaji wa sampuli mbalimbali za uchunguzi wa Vinasaba vya Binadamu kwa wanafunzi wa Shahada na Stashahada ya polisi (hawapo pichani), katika mafunzo ya usimamizi wa sampuli za jinai kwa Maafisa Polisi yaliyofanyika katika Chuo cha Maafisa wa Polisi Kidatu - mkoani Morogoro, Februari 6, 2026.
Meneja wa Maabara ya Sayansi Jinai Toksikolojia, Dkt. Kagera Ng’weshemi, akiwaelezea wanafunzi wa Shahada na Stashahada ya Polisi (hawapo pichani), namna ukusanyaji, uhifadhi, usafirishaji na utunzaji wa sampuli mbalimbali katika mafunzo ya usimamizi wa sampuli za jinai yaliyofanyika katika Chuo cha Maofisa wa Polisi Kidatu - mkoani Morogoro, Februari 6, 2026.
Baadhi ya wanafunzi wa Shahada na Stashahada ya Polisi, wakifuatilia mawasilisho mbalimbali kutoka kwa Wakufunzi wa mafunzo (hawapo pichani), katika mafunzo ya usimamizi wa Sampuli za jinai kwa Maafisa wa Polisi yaliyofanyika katika Chuo cha Maafisa wa Polisi Kidatu - mkoani Morogoro, Februari 6, 2026.
Baadhi ya wanafunzi wa Shahada na Stashahada ya polisi, wakifanya kazi za vikudi katika mafunzo ya usimamizi wa sampuli za jinai yaliyofanyika katika chuo cha Maafisa wa Polisi Kidatu - mkoani Morogoro, Februari 6, 2026.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka, Christopher Kadio (wa tatu kutoka kulia) akiwa pamoja na Wajumbe wa Bodi alioambatana nao wakipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya NAK Limited, Pamela Mutabazi (katikati) akiwaelezea kuhusu namna uteketezaji wa kemikali taka unavyofanyika mara baada ya kutembelea kampuni hiyo iliyopo Fukayosi, Bagamoyo, Mkoa wa Pwani Februari 3, 2026.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Christopher Kadio (wa tano kutoka kulia) akiwa na Katibu wa Bodi, Dkt. Fidelice Mafumiko (wa tatu kutoka kulia) Wajumbe wa Bodi, Meneja wa Kanda ya Mashariki, Danstan Mkapa (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya NAK Limited, Pamela Mutabazi (wa tano kutoka kushoto) mara baada ya kumaliza kutembelea kampuni hiyo iliyopo Bagamoyo, Pwani.
Mwenyekiti wa Bodi, Christopher Kadio, akikagua baadhi ya kemikali katika ghala la kuhifadhi kemikali la kampuni ya NAK limited inayojihusisha na shughuli ya uteketezaji wa kemikali taka iliyopo Fukayosi, Bagamoyo.
Katibu wa Bodi na Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (wa tatu kutoka kulia) akimuuliza swali Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Bagamoyo Sugar Limited, Sadanand Eravang (wa pili kutoka kushoto) walipotembelea maeneo ya uzalishaji wa sukari katika kiwanda hicho kilichopo Bagamoyo, Mkoa wa Pwani, Februari 3, 2026.