Meneja wa TMDA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Anitha Mshighati, akipata maelezo kuhusu majukumu ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kutoka kwa mtumishi wa Mamlaka, Pascal Mahanju (kushoto) kwenye Maonesho ya Wakulima, Nanenane kwenye viwanja vya John Mwakangale, Agosti 8, 2026.
Mtumishi wa Mamlaka, Jackson Mwijage (kulia) akimuelezea mwananchi majukumu ya Mamlaka kupitia kipeperushi chenye maelezo kuhusu majukumu ya Mamlaka.
Mtumishi wa Mamlaka, Sadiki Ngalowela, akitoa elimu kwa wanafunzi waliotembelea banda la Mamlaka kwenye Maonesho ya Wakulima, Nane nane kwenye viwanja vya John Mwakangale, Agosti 8, 2026.
Mdau kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Mamlaka kwenye Maonesho ya Wakulima, Nanenane kwenye viwanja vya John Mwakangale, Agosti 8, 2026.
Mtumishi wa Mamlaka, Ofisi ya Kanda ya Kati, Hasanati Ally (kushoto) akieleza majukumu ya Mamlaka kwa mwananchi aliyetembelea Banda la Mamlaka katika maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nanenane yanayofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Malecela jijini Dodoma Agosti 1-8, 2026.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete, akizungumza wakati akifungua Paredi ya Mifugo katika maonesho ya Kimataifa ya Wakulima “Nanenane” yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Malecela jijini Dodoma Agosti 5, 2026.
Mtumishi wa Mamlaka, Richard Bundala (aliyeshika Chupa) akieleza majukumu ya Mamlaka kwa wanafunzi waliotembelea banda la Mamlaka katika maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nanenane yanayofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Malecela jijini Dodoma Agosti 1-8, 2026.
Wanafunzi wakipata Elimu baada ya kutembelea banda la Mamlaka katika maonesho ya Kimataifa ya Wakulima Nanenane yanayofanyika katika Viwanja vya Dkt. John Malecela jijini Dodoma Agosti 1-8, 2026.
Kaimu Mkemia Mkuu wa Serikali, Daniel Ndiyo, akizungumza wakati akiwakaribisha wadau wa kemikali aina ya Sulphur katika kikao cha wadau hao kilichofanyika katika ukumbi wa Hazina Dar es Salaam Julai 24, 2026.
Meneja wa Ukaguzi wa kemikali na Maabara za Kemia, Gerald Meliyo, akizungumza wakati akimkaribisha Kaimu Mkemia Mkuu wa Serikali, kufungua kikao cha wadau wa kemikali aina ya Sulphur kilichofanyika katika ukumbi wa Hazina Dar es Salaam Julai 24, 2026.