Mkurugenzi wa Huduma za Sayansi Jinai, David Elias (aliyesimama) akizungumza wakati akifungua mafunzo ya Wachunguzi wa Maabara za Sayansi Jinai na Vinasaba vya Binadamu, yanayofanyika katika Jengo la Mkemia, Dar es Salaam, kuanzia tarehe 26–28 Agosti 2026.
Mkurugenzi wa Huduma za Sayansi Jinai, David Elias (aliyekaa katikati) akiwa pamoja na washiriki wa mafunzo ya Wachunguzi wa Maabara za Sayansi Jinai na Vinasaba vya Binadamu, mara baada ya ufunguzi wa mafunzo hayo yaliyofanyika katika Jengo la Mkemia, Dar es Salaam.
Mwezeshaji wa mafunzo, Dkt. Victor Makene, kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akiwasilisha mada katika mafunzo ya Wachunguzi wa Maabara za Sayansi Jinai na Vinasaba vya Binadamu.
Meneja wa Sehemu ya Usajili na Ukaguzi wa Maabara za Sayansi Jinai na Vinasaba vya Binadamu, Fidelis Segumba, akiwasilisha mada kuhusu Sheria ya Udhibiti wa Vinasaba vya Binadamu ya Mwaka 2009 wakati wa mafunzo ya Wachunguzi wa Maabara za Sayansi Jinai na Vinasaba vya Binadamu.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo wakifuatilia uwasilishaji wa mada mbalimbali katika mafunzo ya Wachunguzi wa Maabara za Sayansi Jinai na Vinasaba vya Binadamu yanayofanyika ukumbi wa Mkemia, Dar es Salaam.
Mkemia Mkuu wa Serikali Dkt. Fidelice Mafumiko (katikati), akimpokea Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI, Mhe. Dkt. Zeyana Abdallah Hamid (wa pili kushoto), wakati wajumbe wa Kamati hiyo walipotembelea Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Makao Makuu, Dodoma, Septemba 4, 2026.
Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti, Dkt. Zeyana Abdallah Hamid (aliyevaa hijab) wakimsikiliza Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (kulia), baada ya kuwapokea walipowasili Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Dodoma kwa ziara ya kikazi iliyofanyika Septemba 4, 2026.
Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti, Dkt. Zeyana Abdallah Hamid (kulia) wakimsikiliza Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (kulia), mara baada ya kutembelea ofisi ya mapokezi ya Sampuli wakati ws ziara yao katika Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Dodoma, Septemba 4, 2026.
Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti, Dkt. Zeyana Abdallah Hamid (kulia) wakimsikiliza Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (kulia), mara baada ya kutembelea ofisi ya mapokezi ya Sampuli wakati ws ziara yao katika Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Dodoma, Septemba 4, 2026.
Mtumishi wa Mamlaka ambaye ni msimamizi wa ofisi za mapokezi ya sampuli, Muhsin Kilonzo (kulia), akitoa ufafanuzi kwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI namna wanavyopokea sampuli na kuzifanyia kazi wakati wajumbe hao walipotembelea Mamlaka, Makao Makuu, Dodoma, Septemba 4, 2026.