Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (aliyesimama), akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Kanda ya Mashariki wakati wa kikao kazi cha kuwapongeza kwa kufikia malengo ya makusanyo ya mwaka 2025/2026 kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Kanda ya Mashariki, jijini Dar es Salaam, Agosti 15, 2026. Kulia ni Meneja Ofisi ya Kanda ya Mashariki, Danstan Mkapa.
Meneja Ofisi ya Kanda ya Mashariki, Danstan Mkapa (aliyesimama), akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (kushoto), kwenye kikao kazi cha watumishi wa Ofisi ya Kanda ya Mashariki kilichofanyika katika jengo la ushirika, jijini Dar es Salaam, Agosti 15,2026.
Watumishi wa Mamlaka, wakipokea maelekezo kutoka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (hayupo pichani), katika kakao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Kanda ya Mashariki, jijini Dar es Salaam, Agosti 15, 2026.
Msimamizi wa Dawati la Uhasibu na Utawala wa Ofisi ya Kanda ya Mashariki, Sophia Nuru, akipokea pongezi kutoka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (hayupo pichani), kwa usimamizi mzuri wa mapato katika kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Kanda ya Mashariki, jijini Dar es Salaam, Agosti 15, 2026.
Msimamizi wa Dawati la Usajli na Vibali, Leocardia Magere , akipokea pongezi kutoka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (hayupo pichani), kwa kazi kubwa na nzuri anayoisimamia katika dawati hilo wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Kanda ya Mashariki, jijini Dar es Salaam, Agosti 15, 2026.
Msimamizi wa Dawati la Ukaguzi wa Shehena za Kemikali, Jeremiah Nkulukulu, akipokea pongezi kutoka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (hayupo pichani), kwa kazi kubwa na nzuri anayoisimamia katika dawati hilo wakati wa kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Kanda ya Mashariki, jijini Dar es Salaam, Agosti 15, 2026.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma, Sylvester Omary, akichangia hoja kuhusu kujitangaza zaidi kwa wadau ili kuilinda na kuiimarisha taswira ya taasisi nje ya taasisi, katika kikao cha watumishi wa Ofisi ya Kanda ya Mashariki kilichofanyika jijini Dar es Salaam, Agosti 15, 2026.
Katibu wa Mkemia Mkuu wa Serikali, Dorothy Shija, akiwakumbusha Watumishi wa Ofisi ya Kanda ya Mashariki kuhusu masuala ya kiutawala na vibali vya safari za nje katika kikao kazi kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Kanda ya Mashariki, jijini Dar es Salaam, Agosti 15, 2026.
Meneja wa TMDA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Anitha Mshighati, akipata maelezo kuhusu majukumu ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kutoka kwa mtumishi wa Mamlaka, Pascal Mahanju (kushoto) kwenye Maonesho ya Wakulima, Nanenane kwenye viwanja vya John Mwakangale, Agosti 8, 2026.
Mtumishi wa Mamlaka, Jackson Mwijage (kulia) akimuelezea mwananchi majukumu ya Mamlaka kupitia kipeperushi chenye maelezo kuhusu majukumu ya Mamlaka.