Waziri wa Afya, Mhe. Mohammed Mchengerwa, akizungumza wakati akifungua Mkutano na Wataalam wa Tiba Asili uliofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji Mtumba, Dodoma, Machi 25, 2026.
Waziri wa Afya, Mhe. Mohammed Mchengerwa (kulia), akimsikiliza Kaimu Meneja wa Maabara ya Maikrobaiolojia, Alois Ngonyani, (kushoto), akitoa maelezo namna Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali inavyofanya kazi katika uchunguzi wa Dawa za Tiba Asili katika Mkutano wa Mhe. Waziri wa Afya na Wataalam wa Tiba Asili uliofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji Mtumba, Dodoma, Machi 25, 2026.
Waziri wa Afya, Mhe. Mohammed Mchengerwa (Katikati), akipata maelezo kuhusu majukumu ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kutoka kwa Mtumishi wa Mamlaka (hayupo pichani) wakati alipotembelea Banda la Mamlaka. Kulia ni Naibu Waziri wa Afya, Mhe. Florence Samizi
Waziri wa Afya, Mhe. Mohammed Mchengerwa (aliyevaa miwani) akitoa maelekezo kuhusu Uchunguzi na Uthibiti wa Dawa za Tiba Asili kwa Wataalamu wa Tiba Asili, wakati alipotembelea Banda la Mamlaka katika mkutano na wataalam wa Tiba Asili uliofanyika Mtumba, Dodoma, Machi 25, 2026
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Moyo Jakaya Kikwete, Dkt. Peter Kisenge (kushoto) wakiwa kwenye mkutano wa Waziri wa Afya na Wataalam wa Tiba Asili uliofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji Mtumba, Dodoma, Machi 25, 2026.
Wataalam wa Tiba Asili wakifuatilia Hotuba ya Waziri wa Afya, Mhe. Mohammed Mchengerwa, wakati Mkutano wa Waziri wa Afya na Wataalam wa Tiba Asili uliofanyika Mach 25, 2026, Jijini Dodoma.
Kaimu Meneja wa Maabara ya Maikrobaiolojia, Alois Ngonyani (aliyevaa kofia) akitoa Elimu kwa Wataalamu wa Tiba Asili walipotembelea Banda la Mamlaka kwenye kikao cha Waziri wa Afya na wataalam wa Tiba Asili kilichofanyika Mtumba, Dodoma.
Kaimu Meneja wa Maabara ya Maikrobaiolojia, Alois Ngonyani (aliyevaa kofia) akitoa Elimu kwa Wataalamu wa Tiba Asili walipotembelea Banda la Mamlaka kwenye kikao cha Waziri wa Afya na wataalam wa Tiba Asili kilichofanyika Mtumba, Dodoma.
Mkuu wa wilaya ya Ukerewe, Mhe. Christopher Ngubiagai (aliyesimama), akizungumza wakati akifungua mafunzo kwa waganga wa tiba asili na tiba mbadala yaliyofanyika Machi 27, 2026. Kulia ni Meneja wa Ofisi ya Kanda ya Ziwa, John Wanjala na kushoto ni Kaimu Meneja wa Maabara ya Chakula na Dawa, Everlight Matinga.
Meneja wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Kanda ya Ziwa, John Wanjala, akiwasilisha mada kuhusu mbinu bora za uzalishaji na usafi wa dawa za tiba asili kwenye mafunzo yaliyofanyika Ukerewe, mkoani Mwanza.