Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko, akisaini kitabu cha wageni alipowasili kwemye viwanja vya maonyesho vya Mwalimu Nyerere vilivyopo Barabara ya Kilwa Dar es Salaam Julai 6, 2026.
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (kulia), akisalimiana na Dkt. Garvin Kweka (kushoto), wakati alipotembelea banda la Hospitali ya Taifa Muhimbili kwenye maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) Julai 6,2026.
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (katikati), akizungumza na mtumishi kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na dawa za kulevya (DCEA) (kushoto), wakati alipotembelea banda hilo katika maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) Julai 6,2026. Kulia ni Mkurugenzi wa Uchunguzi wa Bidhaa na Mazingira, Dkt. Shimo Peter.
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (katikati), akipata maelezo kuhusiana na Teknolojia za ujenzi ambazo ni salama kimazingira kutoka kwa mtumishi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jason Moses (kulia), katika maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) Julai 6,2026.
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (kushoto), akipata maelezo kuhusiana na Teknolojia mpya kwa ajili ya upimaji wa Ardhi kutoka kwa mtumishi wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi (kulia), katika maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) Julai 6,2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akizungumza wakati akifungua maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yaliyofanyika katika viwanja vya maonesho vya Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam, Julai 3,2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, (wa pili kutoka kulia) akiwa ameongozana na Rais wa Msumbiji, Mhe. Daniel Chapo (Katikati) walipowasili katika viwanja vya maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) kwa ajili ya ufunguzi rasmi uliofanyika Julai 3,2026.
Mkurugenzi wa Huduma za Taasisi, Evaclotida Kapinga (Katikati), akiwa pamoja na watumishi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwenye banda la Mamlaka katika maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) Julai 3, 2026.
Mtumishi wa Mamlaka, Michael Benarnard (kushoto), akieleza kuhusu majukumu ya Mamlaka kwa mwananchi aliyetembelea Banda la Mamlaka katika maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) Julai 3, 2026.
Mtumishi wa Mamlaka, Victoria Kyara (kulia), akieleza kuhusu majukumu mbalimbali ya Mamlaka kwa mwananchi aliyetembelea Banda la Mamlaka katika maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba) Julai 3, 2026.