Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, Yusuph Mwenda (wa pili kutoka kushoto), akikabidhi cheti cha heshima cha Forodha kwa Meneja wa Ofisi ya Kanda Mashariki Danstan Mkapa (katikati), ambaye alipokea kwa niaba ya Mkemia Mkuu wa Serikali Dkt. Fidelice Mafumiko katika hafla iliyofanyika ukumbi wa mlimani City Dar es Salaam Januari 26, 2026.
Mkemia Mkuu wa Serikali Dkt. Fidelice Mafumiko (kushoto) akipokea Cheti cha heshima cha Forodha kutoka kwa Meneja wa Mamlaka, Ofisi ya Kanda ya Mashariki Danstan Mkapa (kulia), ambaye alimuwakilisha kupokea cheti hicho kilichotolewa na Shirika la Forodha Duniani katika hafla iliyofanyika ukumbi wa mlimani City Dar es Salaam Januari 26, 2026. Mkemia Mkuu wa Serikali alikabidhiwa cheti hicho ofisini kwake Dodoma, Januari 27, 2026.
Cheti cha heshima cha Forodha kilichokabidhiwa kwa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali na Shirika la Forodha Duniani kwa kutambua na kuthamini mchango wake wa utoaji huduma wa kipekee kwa jumuiya ya Kimataifa ya forodha katika hafla iliyofanyika ukumbi wa mlimani City Dar es Salaam Januari 26, 2026.
Meneja wa Ofisi ya Kanda ya Mashariki, Danstan Mkapa (kushoto) akiwa pamoja na Msimamizi wa Dawati la Usajili na Vibali, Kanda ya Mashariki, Leocardia Magere (kulia) wakiwa na cheti kilichotolewa na Shirika la Forodha Duniani kwa kutambua mchango wa Mamlaka katika masuala ya Forodha kilichokabidhiwa na TRA katika hafla iliyofanyika ukumbi wa mlimani City Dar es Salaam Januari 26, 2026.
Meneja wa Mamlaka, Ofisi ya Kanda ya Ziwa, John Wanjala, akielezea majukumu ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali baada ya kufungua mafunzo kwa madereva wanaosafirisha kemikali yaliyofanyika katika ukumbi wa TMDA jijini Mwanza Januari 16, 2026.
Sane Lyochi kutoka Ofisi ya Kanda ya Ziwa, akiwasilisha mada kuhusu madhara ya kemikali kwa madereva wanaosafirisha mizigo hatarishi ya kemikali wakati wa mafunzo ya usafirishaji salama wa kemikali yaliyofanyika jijini Mwanza.
Washiriki wa mafunzo ya usafirishaji salama wa kemikali wakifuatilia mada mbalimbali zilizowasilishwa na wawezeshaji kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Kanda ya Ziwa.
Sane Lyochi kutoka Ofisi ya Kanda ya Ziwa, akiwasilisha mada kuhusu madhara ya kemikali kwa madereva wanaosafirisha mizigo hatarishi ya kemikali wakati wa mafunzo ya usafirishaji salama wa kemikali yaliyofanyika jijini Mwanza.
Askari kutoka Jeshi la Polisi, kutoka Ofisi ya Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Mwanza, Christopher Miku, akitoa elimu kuhusu Sheria ya Usalama barabarani kwa madereva walioshiriki mafunzo ya usafirishaji salama wa kemikali yaliyofanyika jijini Mwanza.
Meneja wa Mamlaka, Ofisi ya Kanda ya Ziwa, John Wanjala (aliyekaa katikati) akiwa na wawezeshaji pamoja na madereva wanaosafirisha kemikali baada ya ufunguzi wa mafunzo ya usafirishaji salama wa kemikali yaliyofanyika jijini Mwanza Januari 15, 2026.