Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu), Zuhura Yunus (kulia) akipata maelezo kuhusu majukumu ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kutoka kwa Meneja wa Mamlaka Ofisi ya Kanda ya Kaskazini, Eliamini Mkenga alipotembelea banda la Mamlaka katika Maonesho ya Kitaifa ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi yanayoendelea katika viwanja vya Mandewa mkoani Singida kuanzia Aprili 24 hadi Aprili 30, 2025.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego (kulia) akisaini kitabu cha wageni huku akipata maelezo kuhusu majukumu ya Mamlaka kutoka kwa mtumishi wa Mamlaka, Saile Kurata (kushoto) alipotembelea banda la Mamlaka katika Maonesho ya Kitaifa ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi yanayofanyika katika viwanja vya Mandewa mkoani Singida Aprili 26, 2025.
Mtumishi wa Mamlaka, Alice Mushi (kushoto), kutoka Mamlaka, Makao Makuu Dodoma akihudumia mdau aliyetembelea banda la Mamlaka katika Maonesho ya Kitaifa ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi yanayoendelea katika viwanja vya Mandewa Mkoani Singida.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka, Profesa Edda Vuhahula (katikati), Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (wa tatu kushoto), Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP), Saleh Ambika (wa tatu kulia) na watumishi walioambatana nao wakiwa pamoja na watumishi wa taasisi za Serikali zilizopo katika Mpaka wa Namanga mara baada ya kumaliza kikao na watumishi hao kilichofanyika katika Mpaka wa Namanga uliopo katika Wilaya ya Longido, Mkoa wa Arusha, Machi 26, 2025.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka, Profesa Edda Vuhahula, Mjumbe wa Bodi, Naibu Kamishna wa Polisi, Saleh Ambika na Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko wakikagua ujenzi wa nyumba ya makazi ya watumishi katika mpaka wa Namanga ambayo inatarajiwa kukamilika ndani ya mwezi Aprili, 2025.
Afisa Mnadhimu wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Alfred Hussein (katikati), akiwa pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka, Profesa Said Ali Vuai (wa tatu kulia), Lusajo Ndagile (wa tatu kushoto), Meneja wa Usajili wa Kemikali na Maabara za Kemia, Musa Kuzumila (wa pili kulia), Mkuu wa Upelelezi wa Polisi Jinai Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Ramia Mganga (kulia), pamoja na watumishi wa Mamlaka na wa jeshi la Polisi Mkoa wa Ruvuma, Machi 27,2025.
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Songea (Souwasa), Mhandisi Jafari Yahaya (wa tatu kulia), akitoa maelezo kwa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka pamoja na watumishi walioambatana nao kuhusu sehehemu ambayo maji yanatibiwa kabla ya kwenda kwa watumiaji mara baada ya kutembelea eneo hilo lililopo Mkoa wa Ruvuma, Machi 27, 2025.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi, Dkt. Batilda Burian (kushoto) akiongea na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka, Profesa Edda Vuhahula (kulia) na ujumbe alioongozana nao (hawapo pichani) mara baada ya kufika katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tanga kwa ajili ya kusalimia na kumfahamisha kuhusu ziara yao ya kikazi katika Mkoa huo, Machi 24, 2025.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka, Profesa Edda Vuhahula (aliyekaa kushoto,) na Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (aliyekaa kulia,) wakiongea na Meneja wa Bandari ya Tanga, Masoud Mrisha (aliyekaa katikati) mara baada ya kufika katika Ofisi ya Bandari Tanga kwa ajili ya ziara ya kikazi, Machi 24, 2025.
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Mamlaka, Dkt. Fidelice Mafumiko (katikati) akizungumza katika siku ya pili ya kikao cha Kwanza cha Baraza la Nane la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kilichofanyika katika ukumbi wa Dkt. Mafumiko jijini Dodoma Machi 29, 2025