Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

MAMLAKA YA MAABARA YA MKEMIA MKUU WA SERIKALI

GCLA Logo
ISO 9001:2015 Certified

Sehemu ya Usajili na Ukaguzi wa Maabara za Sayansi Jinai na Vinasaba vya Binadamu

Sehemu hii inafanya kazi zifuatazo:

  • Kutayarisha Miongozo, Mipango ya ukaguzi na dodoso kwa ajili ya usajili na ukaguzi wa Maabara za Sayansi Jinai na Vinasaba vya Binadamu;
  • Kuratibu na kufanya ukaguzi wa Maabara za Sayansi Jinai na Vinasaba vya Binadamu;
  • Kutoa vyeti au leseni za usajili wa Maabara za Sayansi Jinai na Vinasaba vya Binadamu;
  • Kutunza na kutangaza kwenye Gazeti la Serikali Maabara za Sayansi Jinai na Vinasaba vya Binadamu;
  • Kuratibu Mikutano ya Kamati ya Kitaalam ya Maabara za Sayansi Jinai na Vinasaba vya Binadamu;
  • Kuratibu na kutekeleza Itifaki ya Montreal inayohusu kulinda tabaka la Ozoni;
  • Kufanya mafunzo maalum kwa Wakaguzi wa Maabara za Sayansi Jinai na Vinasaba vya Binadamu na kuwatangaza kwenye Gazeti la Serikali;
  • Kupendekeza Kanuni mpya na kufanya mapitio ya Kanuni zinazohusiana na kemikali na maabara za kemia;
  • Kuratibu uandaaji na utekelezaji wa sera za kemikali, tafiti au programu za kitaifa na kimataifa; na
  • Kufuatilia utekelezaji wa matakwa ya Sheria ya Udhibiti wa Vinasaba vya Binadamu na Kanuni zake.