Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

MAMLAKA YA MAABARA YA MKEMIA MKUU WA SERIKALI

GCLA Logo
ISO 9001:2015 Certified

Sehemu ya Usimamizi wa Rasilimali Watu na Utawala

Sehemu hii inafanya kazi zifuatazo: -

  • Utekelezaji wa Sera na Mikakati ya Rasilimali Watu;
  • Kusaidia kutafsiri na utekelezaji wa Sheria za Utumishi wa Umma, Sheria ya Wakala wa Serikali na Kanuni zake, Miongozo ya kiutumishi na Sheria za Kazi;
  • Kusimamia uhusiano na ustawi wa Watumishi ikiwemo usalama wa afya, malipo ya uzeeni, michezo na utamaduni;
  • Kuratibu na kusimamia Masjala, Kumbukumbu za Ofisi na huduma za Uongozi na Usambazaji wa Vifurushi na Nyaraka;
  • Kusimamia huduma za ulinzi, usafiri na matumizi ya ofisi kwa ujumla;
  • Usimamizi wa ujumla wa matengenezo ikiwemo matengenezo ya vifaa vya ofisi, majengo na maeneo ya ofisi;
  • Kutekeleza masuala mtambuka ikiwemo Jinsia, Kuzuia Rushwa, Maadili, wasiojiweza, VVU/UKIMWI na mambo mengine yanayohusiana na hayo;
  • Kuratibu na kusimamia utekelezaji wa Ushiriki wa Sekta Binafsi katika Shughuli za Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali.
  • Kuratibu na kusimamia masuala yanayohusu ushiriki wa Watumishi katika Shughuli za Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali;
  • Kuwezesha mafunzo na maendeleo ya Rasilimali Watu;
  • Kuandaa na kutekeleza mipango ya Rasilimali Watu;
  • Kusimamia mishahara na malipo ya mishahara; na
  • Kuandaa mipango na bajeti ya mishahara ya Watumishi ya mwaka.