Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

MAMLAKA YA MAABARA YA MKEMIA MKUU WA SERIKALI

GCLA Logo
ISO 9001:2015 Certified

Kitengo TEHAMA na Takwimu

Kitengo hiki kinafanya kazi zifuatazo: -

  • Kusimamia na kupanga mtandao kwa matumizi ya sasa na baadae pamoja na kutengeneza mifumo na kanzidata kutegemeana na mahitaji
  • Usimamizi, utunzaji na urudishaji wa taarifa wakati wa utengenzaji na utekelezaji wa majaribio ya mifumo mara kwa mara;
  • Usimamizi wa usimikaji, ufungaji, uboreshaji, na uhamishaji wa programu ya kanzidata na matoleo mapya yanayohusiana na programu hiyo pia kuhamisha taarifa kutoka Server za zamani kupeleka Server mpya;
  • kuidhinisha utekelezaji wa mabadiliko ya usanidi kwa mitandao ya nje na ndani;
  • Kuandaa na kuelekeza sera ya TEHAMA na mipango mkakati ya maendeleo inayohusiana na Miundombinu ya Mtandao;
  • Kutoa uangalizi wa kiufundi na mwongozo kwa mifumo na miundombinu yote ya kituo cha data;
  • Kuwezesha usambazaji wa maarifa yanayohusiana na TEHAMA kwa Watumishi wa Mamlaka;
  • Kusaidia katika kubuni na uunganishaji wa mifumo na kuhakikisha utangamano wa mifumo iliyopo na miundombinu ya mtandao;
  • Usimamizi wa mchakato wa mabadiliko ya usanidi na kutoa taarifa ya kukatika kwa mtandao;
  • Kutengeneza zana na mbinu rahisi za ufikiaji  wa data, takwimu na ripoti;
  • Kuwezesha ukusanyaji, uchambuzi na kutayarisha ripoti juu ya takwimu za Mamlaka;
  • Kuratibu ukusanyaji na uchambuzi wa data na uandaaji wa  takwimu zinazohusiana na sekta;
  • Kusimamia na kuhakikisha utekelezaji wa  nyaraka zinazohusiana na usalama wa TEHAMA
  • Kuchambua na kutafsiri takwimu ili kutambua umuhimu kuhusiana na vyanzo vya taarifa; na
  • Kutunza data za Mamlaka