Meneja wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Kanda ya Kati, Gerald Mollel, akieleza majukumu ya Mamlaka katika mafunzo ya matumizi na utunzaji sahihi wa kemikali ya Zebaki kwa wachimbaji wa Dhahabu katika mgodi wa Sekenke, yaliyofanyika katika ukumbi wa Wasafi, uliopo Shelui mkoani Singida Februari 7, 2025.
Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Singida, Mhandisi Sabai Nyasili, akitoa shukrani kwa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Kanda ya Kati kwa kutoa mafunzo ya matumizi na utunzaji sahihi wa kemikali ya Zebaki kwa wachimbaji wa Dhahabu katika mgodi wa Sekenke, yaliyofanyika katika ukumbi wa Wasafi, Shelui mkoani Singida Februari 7, 2025.
Mtumishi wa Mamlaka, Revocatus Mwamba (aliyesimama) akiwasilisha mada juu ya Madhara ya Zebaki katika mafunzo ya matumizi na utunzaji sahihi wa kemikali ya Zebaki kwa wachimbaji wa Dhahabu katika mgodi wa Sekenke, yaliyofanyika katika ukumbi wa Wasafi, Shelui mkoani Singida Februari 7, 2025.
Wachimbaji wa Dhahabu wanaotumia kemikali ya Zebaki katika mgodi wa Sekenke wakifuatilia mada mbalimbali katika mafunzo ya matumizi na utunzaji sahihi wa kemikali ya Zebaki yaliyofanyika katika ukumbi wa Wasafi, Shelui mkoani Singida Februari 7, 2025.
Meneja wa Ofisi ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Kanda ya Mashariki, Danstan Mkapa (aliyesimama) akizungumza wakati akifungua Mafunzo kwa madereva wanaosafirisha Kemikali yaliyofanyika katika Ukumbi wa jengo la Ushirika, jijini Dar es Salaam, Februari 8,2025.
Msimamizi wa Dawati la Usajili na Vibali, Ofisi ya Kanda ya Mashariki, Stafford Mwasilonda (aliyesimama) akizungumza kabla ya Kumkaribisha Meneja wa Ofisi ya Kanda ya Mashariki, Danstan Mkapa (kulia), kufungua mafunzo kwa Madereva wanaosafirisha Kemikali yaliyofanyika Ukumbi wa jengo la Ushirika, Februari 8,2025.
Msimamizi wa Dawati la Ukaguzi, Ofisi ya Kanda ya Mashariki, Jeremiah Nkulukulu, akiwasilisha mada kuhusu Madhara ya Kemikali kwa Afya na Mazingira kwenye mafunzo ya Madereva wanaosafirisha Kemikali yaliyofanyika katika Ukumbi wa Jengo la Ushirika, jijini Dar es Salaam, Februari 8,2025.
Baadhi ya Madereva wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na Watumishi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali katika mafunzo ya Madereva wanaosafirisha Kemikali yaliyofanyika katika Ukumbi wa Jengo la Ushirika, jijini Dar es Salaam, Februari 8,2025.
.
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro, Murtallah Sadiki (kushoto) akisaini kitabu cha wageni mbele ya Mtumishi wa Mamlaka, Sadock Mboya (kulia) wakati alipotembelea banda la Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwenye maonesho ya wiki ya Sheria katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara, Abeid Kafunda (kushoto) akisaini kitabu cha wageni mbele ya Mtumishi wa Mamlaka, Sadock Mboya (kulia) wakati alipotembelea banda la Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwenye maonesho ya wiki ya Sheria katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.