Meneja wa Mamlaka, Ofisi ya Kanda ya Ziwa, John Wanjala, akielezea majukumu ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali baada ya kufungua mafunzo kwa madereva wanaosafirisha kemikali yaliyofanyika katika ukumbi wa TMDA jijini Mwanza Januari 16, 2026.
Sane Lyochi kutoka Ofisi ya Kanda ya Ziwa, akiwasilisha mada kuhusu madhara ya kemikali kwa madereva wanaosafirisha mizigo hatarishi ya kemikali wakati wa mafunzo ya usafirishaji salama wa kemikali yaliyofanyika jijini Mwanza.
Washiriki wa mafunzo ya usafirishaji salama wa kemikali wakifuatilia mada mbalimbali zilizowasilishwa na wawezeshaji kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Kanda ya Ziwa.
Sane Lyochi kutoka Ofisi ya Kanda ya Ziwa, akiwasilisha mada kuhusu madhara ya kemikali kwa madereva wanaosafirisha mizigo hatarishi ya kemikali wakati wa mafunzo ya usafirishaji salama wa kemikali yaliyofanyika jijini Mwanza.
Askari kutoka Jeshi la Polisi, kutoka Ofisi ya Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Mwanza, Christopher Miku, akitoa elimu kuhusu Sheria ya Usalama barabarani kwa madereva walioshiriki mafunzo ya usafirishaji salama wa kemikali yaliyofanyika jijini Mwanza.
Meneja wa Mamlaka, Ofisi ya Kanda ya Ziwa, John Wanjala (aliyekaa katikati) akiwa na wawezeshaji pamoja na madereva wanaosafirisha kemikali baada ya ufunguzi wa mafunzo ya usafirishaji salama wa kemikali yaliyofanyika jijini Mwanza Januari 15, 2026.
Meneja wa Mamlaka Ofisi ya Kanda ya Ziwa, John Wanjala, akielezea majukumu ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali baada ya kufungua mafunzo kwa wasimamizi wa kemikali yaliyofanyika katika ukumbi wa TMDA jijini Mwanza Januari 14, 2026.
Washiriki wa mafunzo ya usimamizi salama ya kemikali wakifuatilia mada mbalimbali zilizowasilishwa na wawezeshaji kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Ofisi ya Kanda ya Ziwa.
Mtumishi wa Mamlaka, Ofisi ya Kanda ya Ziwa, Sane Lyochi, akiwasilisha mada kuhusu utaratibu wa uteketezaji wa kemikali na kemikali taka kwa wasimamizi wa kemikali walioshiriki mafunzo ya usimamizi salama wa kemikali yaliyofanyika jijini Mwanza.
Mtumishi wa Mamlaka, Ofisi ya Kanda ya Ziwa, Boaz Mizar, akiwasilisha mada kuhusu utambuzi na mawasiliano ya uhatarishi wa kemikali wakati wa mafunzo ya usimamizi salama wa kemikali yaliyofanyika jijini Mwanza.